Publicidade

Salmos 113

Kumsifu Mwenyezi Mungu kwa wema wake

1 Msifuni Mwenyezi Mungu..

Enyi watumishi wa Mwenyezi Mungu msifuni,

lisifuni jina la Mwenyezi Mungu.

2 Jina la Mwenyezi Mungu na lisifiwe,

sasa na hata milele.

3 Kuanzia mawio ya jua hadi machweo yake,

jina la Mwenyezi Mungu linapaswa kusifiwa.

4 Mwenyezi Mungu ametukuka juu ya mataifa yote,

utukufu wake juu ya mbingu.

5 Ni nani aliye kama Mwenyezi Mungu, Mungu wetu,

Yule aliyeketi kwenye kiti cha enzi huko juu,

6 ambaye huinama atazame chini

aone mbingu na nchi?

7 Huwainua maskini kutoka mavumbini,

na kuwanyanyua wahitaji

kutoka lundo la majivu,

8 huwaketisha pamoja na wakuu,

pamoja na wakuu wa watu wake.

9 Humjalia mwanamke tasa kutulia nyumbani mwake,

akiwa mama watoto mwenye furaha.

Msifuni Mwenyezi Mungu.

Veja também

Publicidade
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-06-16_18-40-07-