Publicidade

Salmos 16

Sala ya matumaini
Utenzi wa Daudi.

1 Ee Mungu, uniweke salama,

kwa maana kwako nimekimbilia.

2 Nilimwambia Mwenyezi Mungu, "Wewe ndiwe Bwana wangu;

pasipo wewe sina jambo jema."

3 Kuhusu watakatifu walio duniani,

hao ndio wenye fahari,

na ninapendezwa nao.

4 Huzuni itaongezeka kwa wale

wanaokimbilia miungu mingine.

Sitazimimina sadaka za damu kwa miungu kama hiyo,

au kutaja majina yao mdomoni mwangu.

5 Mwenyezi Mungu umeniwekea fungu langu na kikombe changu;

umeyafanya mambo yangu yote yawe salama.

6 Alama za mipaka zimeniangukia mahali pazuri,

hakika nimepata urithi mzuri.

7 Nitamsifu Mwenyezi Mungu ambaye hunishauri,

hata wakati wa usiku moyo wangu hunifundisha.

8 Nimemweka Mwenyezi Mungu mbele yangu daima.

Kwa sababu yuko mkono wangu wa kuume,

sitatikisika.

9 Kwa hiyo moyo wangu unafurahia,

na ulimi wangu unashangilia;

mwili wangu nao

utapumzika salama,

10 kwa maana hutaniacha Kuzimu,

wala hutamwacha Mtakatifu Wako

kuona uharibifu.

11 Umenijulisha njia ya uzima;

utanijaza na furaha mbele zako,

pamoja na furaha ya milele

katika mkono wako wa kuume.

Veja também

Publicidade
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-06-16_06-50-08-