Publicidade

Salmos 84

Kuionea shauku nyumba ya Mwenyezi Mungu
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa gitithi. Zaburi ya wana wa Kora.

1 Ee Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni,

makao yako yapendeza kama nini!

2 Nafsi yangu inatamani sana,

naam, hata kuona shauku,

kwa ajili ya nyua za Mwenyezi Mungu;

moyo wangu na mwili wangu

vinamlilia Mungu Aliye Hai.

3 Hata shomoro amejipatia makao,

mbayuwayu amejipatia kiota

mahali awezapo kuweka makinda yake:

mahali karibu na madhabahu yako,

Ee Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni,

Mfalme wangu na Mungu wangu.

4 Heri wale wanaokaa nyumbani mwako,

wanaokusifu wewe daima.

5 Heri wale ambao nguvu zao ziko kwako,

na njia ziendazo Sayuni zimo mioyoni mwao.

6 Wanapopita katika Bonde la Baka,

hulifanya mahali pa chemchemi,

pia mvua za vuli hulijaza kwa madimbwi.

7 Huendelea toka nguvu hadi nguvu,

hadi kila mmoja afikapo

mbele za Mungu huko Sayuni.

8 Ee Bwana Mwenyezi Mungu,

Mungu wa majeshi ya mbinguni,

sikia maombi yangu;

nisikilize, Ee Mungu wa Yakobo.

9 Ee Mungu, uitazame ngao yetu,

mtazame kwa wema mpakwa mafuta wako.

10 Siku moja katika nyua zako ni bora

kuliko siku elfu mahali pengine;

afadhali ningekuwa bawabu katika nyumba ya Mungu wangu

kuliko kukaa katika mahema ya waovu.

11 Kwa kuwa Bwana Mwenyezi Mungu ni jua na ngao;

Mwenyezi Mungu hutoa wema na heshima;

hakuna kitu chema anachowanyima

wale ambao hawana hatia.

12 Ee Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni,

heri mtu anayekutumaini wewe.

Veja também

Publicidade
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-06-16_06-50-08-