Pular para o conteúdo
Publicidade

Zaburi 123

Kuomba rehema

Wimbo wa kwenda juu.

1 Ninayainua macho yangu kwako,

kwako wewe unayeketi mbinguni kwenye kiti chako cha enzi.

2 Kama vile macho ya watumwa

yatazamavyo mkono wa bwana wao,

kama vile macho ya mjakazi

yatazamavyo mkono wa bibi yake,

ndivyo macho yetu yamtazamavyo Mwenyezi Mungu, Mungu wetu,

hadi atakapotuhurumia.

3 Uturehemu, Ee Mwenyezi Mungu, uturehemu,

kwa maana tumevumilia dharau nyingi.

4 Tumevumilia dhihaka nyingi kutoka kwa wenye kiburi,

dharau nyingi kutoka kwa wenye majivuno.

Estes versículos te tocaram? Ore agora!

+581 estão orando agora.

Junte-se à corrente de oração.

Veja também