Publicidade

Salmos 53

Uovu wa wanadamu
Kwa mwimbishaji. Mtindo wa mahalathi. Utenzi wa Daudi.

1 Mpumbavu anasema moyoni mwake,

"Hakuna Mungu."

Wameharibika, na njia zao ni za uovu kabisa,

hakuna hata mmoja atendaye mema.

2 Mungu anawachungulia wanadamu chini

kutoka mbinguni

aone kama wako wenye akili,

wowote wanaomtafuta Mungu.

3 Kila mmoja amegeukia mbali,

wameharibika wote pamoja,

hakuna atendaye mema.

Naam, hakuna hata mmoja!

4 Je, watendao maovu kamwe hawatajifunza:

wale ambao huwala watu wangu

kama watu walavyo mkate,

hao ambao hawamwiti Mungu?

5 Hapo waliingiwa na hofu kuu,

ambapo hapakuwa na hofu.

Mungu alitawanya mifupa ya wale waliokushambulia;

uliwaaibisha, kwa sababu Mungu aliwadharau.

6 Laiti wokovu wa Israeli ungekuja kutoka Sayuni!

Mungu anaporejesha wafungwa wa watu wake,

Yakobo na ashangilie, Israeli na afurahi!

Veja também

Publicidade
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-06-16_18-40-07-