Pular para o conteúdo
Publicidade

Zaburi 131

Kumtegemea Mwenyezi Mungu kwa unyenyekevu

Wimbo wa kwenda juu. Wa Daudi.

1 Moyo wangu hauna kiburi, Ee Mwenyezi Mungu,

macho yangu hayajivuni;

sijishughulishi na mambo makuu kunizidi

wala mambo ya ajabu mno kwangu.

2 Lakini nimetuliza na kunyamazisha nafsi yangu;

kama mtoto aliyeachishwa kunyonya na mama yake,

kama mtoto aliyeachishwa kunyonya

ndivyo ilivyo nafsi iliyo ndani yangu.

3 Ee Israeli, mtumaini Mwenyezi Mungu

tangu sasa na hata milele.

Estes versículos te tocaram? Ore agora!

+581 estão orando agora.

Junte-se à corrente de oração.

Veja também