Publicidade

Salmos 120

Kuomba msaada dhidi ya wadanganyifu
Wimbo wa kwenda juu.

1 Katika dhiki yangu namwita Mwenyezi Mungu,

naye hunijibu.

2 Ee Mwenyezi Mungu, uniokoe kutoka midomo ya uongo

na ndimi za udanganyifu.

3 Atakufanyia nini,

au akufanyie nini zaidi, ewe ulimi mdanganyifu?

4 Atakuadhibu kwa mishale mikali ya shujaa,

kwa makaa yanayowaka ya mti wa mretemu.

5 Ole wangu kwa kuwa naishi Mesheki,

kwamba naishi katikati ya mahema ya Kedari!

6 Nimeishi muda mrefu mno

miongoni mwa wale wanaochukia amani.

7 Mimi ni mtu wa amani;

lakini ninaposema, wao wanataka vita.

Veja também

Publicidade
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-06-18_14-04-22-