Publicidade

Salmos 142

Maombi ya kuokolewa dhidi ya watesi
Utenzi wa Daudi. Alipokuwa pangoni. Maombi.

1 Namlilia Mwenyezi Mungu kwa sauti,

napaza sauti yangu kwa Mwenyezi Mungu anihurumie.

2 Namimina malalamiko yangu mbele zake,

mbele zake naeleza shida zangu.

3 Roho yangu inapozimia ndani yangu,

wewe ndiwe unajua njia zangu.

Katika njia ninayopita,

watu wameniwekea mtego.

4 Tazama kuume kwangu na uone,

hakuna hata mmoja anayejihusisha nami.

Sina kimbilio,

hakuna anayejali maisha yangu.

5 Ee Mwenyezi Mungu, nakulilia wewe,

nasema, "Wewe ni kimbilio langu,

fungu langu katika nchi ya walio hai."

6 Sikiliza kilio changu,

kwa sababu mimi ni mhitaji sana;

niokoe na wale wanaonifuatilia,

kwa kuwa wamenizidi nguvu.

7 Nifungue kutoka kifungo changu,

ili niweze kulisifu jina lako.

Ndipo wenye haki watanizunguka,

kwa sababu ya wema wako kwangu.

Veja também

Publicidade
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-06-18_14-04-22-