Publicidade

Provérbios 1

1 Mithali za Sulemani mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli:

2 Kwa kupata hekima na nidhamu;

kwa kufahamu maneno ya busara;

3 kwa kujipatia nidhamu na busara,

kufanya lililo sawa, haki na bila kupendelea;

4 huwapa busara wajinga1:4 Neno la Kiebrania lililotafsiriwa mjinga (wingi wajinga) linamaanisha mtu anayeamini chochote, asiye na maadili, na mwenye roho ya kutenda uovu.,

maarifa na akili kwa vijana;

5 wenye hekima na wasikilize nao waongeze elimu yao,

wenye kupambanua na wapate mwongozo;

6 kwa kufahamu mithali na mifano,

misemo na vitendawili vya wenye hekima.

7 Kumcha Mwenyezi Mungu ni chanzo cha maarifa,

lakini wapumbavu1:7 Neno la Kiebrania lililotafsiriwa mpumbavu (wingi wapumbavu) linamaanisha mtu asiye na maadili. hudharau hekima na adabu.

Veja também

Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-07-05_19-25-13-