Publicidade

Lamentações 4

Adhabu ya Sayuni

1 Jinsi dhahabu ilivyoacha kung’aa,

Na dhahabu iliyo safi ilivyobadilika!

Mawe ya patakatifu yametupwa

Mwanzo wa kila njia.

2 2 Kor 4:7 Wana wa Sayuni wenye thamani,

Walinganao na dhahabu safi,

Jinsi wanavyodhaniwa kuwa vyombo vya udongo,

Kazi ya mikono ya mfinyanzi!

3 Ayu 39:14 Hata mbwamwitu hutoa matiti,

Huwanyonyesha watoto wao;

Binti ya watu wangu amekuwa mkali,

Mfano wa mbuni jangwani.

4 Zab 22:15 Ulimi wa mtoto anyonyaye

Wagandamana na kinywa chake kwa kiu;

Watoto wachanga waomba chakula,

Wala hakuna hata mmoja awamegeaye.

5 Ayu 24:8;Lk 15:16 Wale waliokula vitu vya anasa

Wameachwa peke yao njiani;

Wale waliokuzwa kuvaa nguo nyekundu

Wakumbatia jaa.

6 Mwa 19:24 Maana uovu wa binti ya watu wangu ni mkubwa

Kuliko dhambi ya Sodoma,

Uliopinduliwa kama katika dakika moja,

Wala mikono haikuwekwa juu yake.

7 Wakuu wake walikuwa safi kuliko theluji,

Walikuwa weupe kuliko maziwa;

Miili yao, walikuwa wekundu kuliko marijani,

Na umbo lao kama yakuti samawi.

8 Zab 102:5 Nyuso zao ni nyeusi kuliko makaa;

Hawajulikani katika njia kuu;

Ngozi yao yagandamana na mifupa yao

Imekauka, imekuwa kama mti.

9 Heri wale waliouawa kwa upanga

Kuliko wao waliouawa kwa njaa;

Maana hao husinyaa, wakichomwa

Kwa kukosa matunda ya mashamba.

10 Omb 2:20;Kum 28:57;Eze 5:10 Mikono ya wanawake wenye huruma

Imewatokosa watoto wao wenyewe;

Walikuwa ndio chakula chao

Katika uharibifu wa binti ya watu wangu.

11 Kum 32:22 BWANA ameitimiza ghadhabu yake,

Ameimimina hasira yake kali;

Naye amewasha moto katika Sayuni

Ulioiteketeza misingi yake.

12 Kum 29:24 Wafalme wa dunia hawakusadiki,

Wala wote wakaao duniani,

Ya kwamba mtesi na adui wangeingia

Katika malango ya Yerusalemu.

13 Yer 5:31;Mt 23:31 Ni kwa sababu ya dhambi za manabii wake

Na maovu ya makuhani wake,

Walioimwaga damu ya wenye haki

Katikati yake.

14 Yer 2:34 Hutangatanga njiani kama vipofu,

Wametiwa unajisi kwa damu;

Hata ikawa hakuna aliyeweza

Kuyagusa mavazi yao.

15 Watu waliwapigia kelele, Ondokeni, Uchafu,

Ondokeni, ondokeni, msiguse;

Walipokimbia na kutangatanga, watu walisema kati ya mataifa,

Hawatakaa hapa tena.

16 Omb 5:12 Hasira ya BWANA imewatenga,

Yeye hatawaangalia tena;

Hawakujali nafsi za wale makuhani,

Hawakuwaheshimu wazee wao.

17 2 Fal 24:7;Isa 20:5,6 Macho yetu yamechoka

Kwa kuutazamia bure msaada wetu;

Katika kungoja kwetu tumengojea taifa

Lisiloweza kutuokoa.

18 2 Fal 25:4;Yer 51:33 Wanatuvizia hatua zetu,

Hata hatuwezi kwenda katika njia zetu;

Mwisho wetu umekaribia, siku zetu zimetimia;

Maana mwisho wetu umefika.

19 Waliotufuatia ni wepesi

Kuliko tai za mbinguni;

Hao walitufuatia milimani,

Nao walituotea jangwani.

20 Mwa 2:7;Yer 52:9 Pumzi ya mianzi ya pua zetu, masihi4:20 Au, mtiwa mafuta (tazama 1 Sam 2:10). wa BWANA,

Alikamatwa katika marima yao;

Ambaye kwa habari zake tulisema,

Chini ya kivuli chake tutakaa kati ya mataifa.

21 Furahi, ushangilie, Ee binti Edomu,

Ukaaye katika nchi ya Usi;

Hata kwako kikombe kitapita,

Utalewa, na kujifanya uchi.

22 Adhabu ya uovu wako imetimia, Ee binti Sayuni;

Hatakuhamisha tena;

Atapatiliza uovu wako, Ee binti Edomu;

Atazivumbua dhambi zako.

Veja também

Lamentações
Ver todos os capítulos de Lamentações
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-07-05_19-25-13-