Publicidade

Lamentações 5

Ombi la kuhurumiwa

1 Ee BWANA, kumbuka yaliyotupata;

Utazame na kuiona aibu yetu.

2 Urithi wetu umegeuka kuwa mali ya wageni;

Na nyumba zetu kuwa mali ya mataifa.

3 Tumekuwa yatima waliofiwa na baba;

Mama zetu wamekuwa kama wajane.

4 Tumekunywa maji yetu kwa fedha;

Kuni zetu twauziwa.

5 Watufuatiao wako juu ya shingo zetu;

Tumechoka, tusipate pumziko lolote.

6 Tumewapa hao Wamisri mkono;

Na Waashuri nao, ili tushibe chakula.

7 Baba zetu walitenda dhambi hata hawako;

Na sisi tumeyachukua maovu yao.

8 Watumwa wanatutawala;

Hakuna mtu wa kutuokoa na mikono yao.

9 Twapata chakula kwa kujihatarisha nafsi zetu;

Kwa sababu ya upanga wa nyikani.

10 Ngozi yetu ni nyeusi kama tanuri;

Kwa sababu ya joto ya njaa ituteketezayo.

11 Wanawake katika Sayuni wanashikwa kwa nguvu;

Na mabikira katika miji ya Yuda.

12 Wakuu hutundikwa kwa mikono yao;

Nyuso za wazee hazipewi heshima.

13 Vijana huyachukua mawe ya kusagia;

Na watoto hujikwaa chini ya kuni.

14 Wazee wameacha kwenda langoni;

Na vijana kwenda ngomani.

15 Furaha ya mioyo yetu imekoma;

Machezo yetu yamegeuka maombolezo.

16 Taji ya kichwa chetu imeanguka;

Ole wetu! Kwa kuwa tumetenda dhambi.

17 Kwa sababu hiyo mioyo yetu imezimia;

Kwa ajili ya hayo macho yetu hayaoni vema.

18 Kwa ajili ya mlima Sayuni ulio ukiwa,

Mbweha hutembea juu yake.

19 Wewe, BWANA, unadumu milele;

Kiti chako cha enzi ni tangu kizazi hata kizazi.

20 Mbona watusahau sikuzote;

Na kutuacha muda huu mwingi?

21 Ee BWANA, utugeuze kwako, nasi tutageuka; Zifanye mpya siku zetu kama siku za kale.

22 Ingawa wewe umetukataa kabisa;

Nawe una hasira nyingi sana juu yetu.

Veja também

Publicidade
Lamentações
Ver todos os capítulos de Lamentações
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-06-15_21-32-39-