Pular para o conteúdo
Publicidade

Isaías 40

28 Je wewe, hufahamu?

Je wewe, hujasikia?

Mwenyezi Mungu ni Mungu wa milele,

Muumba wa miisho ya dunia.

Hatachoka wala kulegea,

wala hakuna hata mmoja

awezaye kuupima ufahamu wake.

29 Huwapa nguvu waliolegea

na huongeza nguvu za wadhaifu.

30 Hata vijana huchoka na kulegea,

nao vijana wanaume hujikwaa na kuanguka,

31 bali wale wamtumainio Mwenyezi Mungu

atafanya upya nguvu zao.

Watapaa juu kwa mabawa kama tai;

watapiga mbio wala hawatachoka,

watatembea kwa miguu wala hawatazimia.

Veja também