4 Hakika alichukua udhaifu wetu
na akajitwika huzuni zetu;
tulidhania kuwa ameadhibiwa na Mungu,
naye akapigwa sana na kujeruhiwa.
5 Lakini alijeruhiwa kwa ajili ya makosa yetu,
alichubuliwa kwa ajili ya maovu yetu;
adhabu iliyotuletea sisi amani ilikuwa juu yake,
na kwa majeraha yake sisi tumepona.