13 "Ukitunza miguu yako isivunje Sabato,
na kutokufanya kama vile upendavyo katika siku yangu takatifu,
ukiita Sabato siku ya furaha
na siku takatifu ya Mwenyezi Mungu ya kuheshimiwa,
kama utaiheshimu kwa kutoenenda
katika njia zako mwenyewe,
na kutokufanya yakupendezayo
au kusema maneno ya upuzi,
14 ndipo utakapojipatia furaha yako katika Mwenyezi Mungu,
nami nitakufanya upande juu ya miinuko ya nchi
na kusherehekea urithi wa Yakobo baba yako."
Kinywa cha Mwenyezi Mungu kimenena haya.