3 na kuwapa mahitaji
wale wanaohuzunika katika Sayuni,
ili kuwapa taji za uzuri badala ya majivu,
mafuta ya furaha badala ya maombolezo,
vazi la sifa badala ya roho ya kukata tamaa.
Nao wataitwa mialoni ya haki,
pando la Mwenyezi Mungu,
ili kuonesha utukufu wake.