6 Kwa maana, kwa ajili yetu mtoto amezaliwa,
tumepewa mtoto wa kiume,
nao utawala utakuwa begani mwake.
Naye ataitwa
Mshauri wa Ajabu, Mungu Mwenye Nguvu,
Baba wa Milele, Mfalme wa Amani.
7 Kuongezeka kwa utawala wake na amani
hakutakuwa na mwisho.
Atatawala kwenye kiti cha utawala cha Daudi
na juu ya ufalme wake,
akiuthibitisha na kuutegemeza
kwa haki na kwa adili,
tangu wakati huo na hata milele.
Wivu wa Mwenyezi Mungu, Mungu wa majeshi ya mbinguni
utatimiza haya.