Publicidade

Provérbios 13

1 1 Sam 2:25;Mit 9:7,8 Mwana mwenye hekima husikiliza mausia ya babaye;

Bali mwenye dharau hasikilizi maonyo.

2 Mtu atakula mema kwa matunda ya kinywa chake;

Bali nafsi ya mtu haini itakula jeuri.

3 Zab 39:1 Yeye alindaye kinywa chake huilinda nafsi yake;

Bali afunuaye midomo yake atapata uharibifu.

4 Nafsi ya mtu mvivu hutamani asipate kitu;

Bali nafsi ya mwenye bidii itanenepeshwa.

5 Kol 3:9;Rum 12:9 Mwenye haki huchukia kusema uongo;

Bali mtu mbaya huwa karaha, hupatwa na aibu.

6 Mit 11:3 Haki humlinda yeye aliye mnyofu katika njia yake;

Bali ubaya humwangusha mwenye dhambi.

7 Kuna mtu anayejitajirisha, lakini hana kitu;

Kuna anayejifanya kuwa maskini, lakini ana mali nyingi.

8 Fidia ya nafsi ya mtu ni utajiri wake;

Bali mtu maskini hasikii ogofyo lolote.

9 Nuru ya mwenye haki yang’aa sana;

Bali taa ya mtu mbaya itazimika.

10 Kiburi huleta mashindano tu;

Bali hekima hukaa nao wanaoshauriana.

11 Mit 20:21 Mali iliyopatikana kwa haraka itapunguka;

Bali yeye achumaye kidogo kidogo atazidishiwa.

12 Kilichotarajiwa kikikawia kuja, moyo huugua.

Bali haja ya mtu ikipatikana, ni mti wa uzima.

13 2 Nya 36:16 Kila anayelidharau neno hujiletea uharibifu;

Bali yeye anayeiogopa amri atapewa thawabu.

14 Mit 16:22;15:24;2 Sam 22:6;Zab 116:3 Sheria ya mwenye akili ni chemchemi ya uzima,

Ili kuepukana na tanzi za mauti.

15 Ufahamu mwema huleta upendeleo;

Bali njia ya muasi huangamiza.

16 Mit 12:23 Kila aliye na busara hutenda kazi kwa maarifa;

Bali mpumbavu hueneza upumbavu.

17 Mjumbe mbaya huanguka maovuni;

Bali mjumbe mwaminifu ni afya.

18 Mit 15:5 Umaskini na fedheha zitampata yeye akataaye kurudiwa;

Bali yeye aangaliaye maonyo ataheshimiwa.

19 Haja iliyopatikana ni tamu nafsini mwa mtu;

Bali kujitenga na maovu ni chukizo kwa wapumbavu.

20 Nenda pamoja na wenye hekima, nawe utakuwa na hekima;

Bali rafiki wa wapumbavu ataumia.

21 Zab 32:10 Uovu huwafuatia wenye dhambi;

Bali mwenye haki atalipwa mema.

22 Mhu 2:26 Mtu mwema huwaachia wana wa wanawe urithi;

Na mali ya mkosaji huwa akiba kwa mwenye haki.

23 Mit 12:11 Chakula kingi chapatikana kwa ukulima wa maskini;

Bali viko viharibiwavyo kwa sababu ya dhuluma.

24 Mit 19:18;22:15 Yeye asiyetumia fimbo yake humchukia mwanawe;

Bali yeye ampendaye humrudi mapema.

25 Mwenye haki hula akaishibisha nafsi yake;

Bali tumbo la mtu mbaya litaona njaa.

Veja também

Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-07-05_12-11-46-