Publicidade

Provérbios 18

1 Ajitengaye na wenzake hutafuta matakwa yake mwenyewe;

Hushindana na kila shauri jema.

2 Mpumbavu hapendezwi na ufahamu;

Ila moyo wake udhihirike tu.

3 Ajapo asiye haki, huja dharau pia;

Na pamoja na aibu huja lawama.

4 Zab 78:2Maneno ya kinywa cha mtu ni kama maji ya vilindi;

Kijito kibubujikacho; chemchemi ya hekima.

5 Law 19:15;Kum 1:17;Ayu 13:7,8;Mit 24:23Kukubali uso wake asiye haki si vizuri;

Wala kumpotosha mwenye haki hukumuni.

6 Midomo ya mpumbavu huingia katika fitina,

Na kinywa chake huita mapigo.

7 Kinywa cha mpumbavu ni uharibifu wake,

Na midomo yake ni mtego wa nafsi yake.

8 Maneno ya mchongezi ni kama vitoweo;

Nayo hushukia pande za ndani za tumbo.

9 Yeye naye aliye mvivu katika kazi yake,

Ni ndugu yake aliye mharibifu.

10 2 Sam 22:3,51;Zab 18:2Jina la BWANA ni ngome imara;

Mwenye haki huikimbilia, akawa salama.

11 Mali ya mtu tajiri ni mji wake wa nguvu;

Ni kama ukuta mrefu katika mawazo yake.

12 Kabla ya uharibifu moyo wa mwanadamu hujivuna;

Na kabla ya heshima hutangulia unyenyekevu.

13 Yeye ajibuye kabla hajasikia,

Ni upumbavu na aibu kwake.

14 Roho ya mtu itastahimili udhaifu wake;

Bali roho iliyovunjika nani awezaye kuistahimili?

Veja também

Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-07-05_19-25-13-