Publicidade

Provérbios 18

1 Ajitengaye na wenzake hutafuta matakwa yake mwenyewe;

Hushindana na kila shauri jema.

2 Mpumbavu hapendezwi na ufahamu;

Ila moyo wake udhihirike tu.

3 Ajapo asiye haki, huja dharau pia;

Na pamoja na aibu huja lawama.

4 Zab 78:2 Maneno ya kinywa cha mtu ni kama maji ya vilindi;

Kijito kibubujikacho; chemchemi ya hekima.

5 Law 19:15;Kum 1:17;Ayu 13:7,8;Mit 24:23 Kukubali uso wake asiye haki si vizuri;

Wala kumpotosha mwenye haki hukumuni.

6 Midomo ya mpumbavu huingia katika fitina,

Na kinywa chake huita mapigo.

7 Kinywa cha mpumbavu ni uharibifu wake,

Na midomo yake ni mtego wa nafsi yake.

8 Maneno ya mchongezi ni kama vitoweo;

Nayo hushukia pande za ndani za tumbo.

9 Yeye naye aliye mvivu katika kazi yake,

Ni ndugu yake aliye mharibifu.

10 2 Sam 22:3,51;Zab 18:2 Jina la BWANA ni ngome imara;

Mwenye haki huikimbilia, akawa salama.

11 Mali ya mtu tajiri ni mji wake wa nguvu;

Ni kama ukuta mrefu katika mawazo yake.

12 Kabla ya uharibifu moyo wa mwanadamu hujivuna;

Na kabla ya heshima hutangulia unyenyekevu.

13 Yeye ajibuye kabla hajasikia,

Ni upumbavu na aibu kwake.

14 Roho ya mtu itastahimili udhaifu wake;

Bali roho iliyovunjika nani awezaye kuistahimili?

15 Efe 1:17 Moyo wa mwenye busara hupata maarifa;

Na sikio la mwenye hekima hutafuta maarifa.

16 Mwa 39:2-6;41:14,38-44;Dan 1:17-20;6:3 Zawadi ya mtu humpatia nafasi;

Humleta mbele ya watu wakuu.

17 Ajiteteaye kwanza huonekana kuwa ana haki;

Lakini jirani yake huja na kumchunguza.

18 Kura hukomesha mashindano;

Hukata maneno ya wakuu.

19 Ndugu aliyechukizwa ni mgumu kuliko mji wa nguvu;

Na mashindano ni kama mapingo ya ngome.

20 Tumbo la mtu litajazwa matunda ya kinywa chake;

Atashiba mazao ya midomo yake.

21 Mt 12:37 Mauti na uzima huwa katika uwezo wa ulimi;

Na wao waupendao watakula matunda yake.

22 Apataye mke apata kitu chema;

Naye ajipatia kibali kwa BWANA.

23 Mwa 42:13-16;Yak 2:3 Maskini hutumia maombi;

Bali tajiri hujibu kwa ukali.

24 Yn 15:14,15 Ajifanyiaye marafiki wengi ni kwa maangamizi yake mwenyewe;

Lakini yuko rafiki aambatanaye na mtu kuliko ndugu.

Veja também

Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-07-04_23-13-58-