Pular para o conteúdo
Publicidade

Provérbios 2

Thamani ya hekima

1 Mwanangu, kama ukiyakubali maneno yangu,

Na kuyaweka akiba maagizo yangu;

2 Hata ukatega sikio lako kusikia hekima,

Ukauelekeza moyo wako upate kufahamu;

3 Naam, ukiita busara,

Na kupaza sauti yako upate ufahamu;

4 Zab 19:10;Mit 3:14,15;Mt 6:19-21Ukiutafuta kama fedha,

Na kuutafutia kama hazina iliyositirika;

5 Ndipo utakapofahamu kumcha BWANA,

Na kupata kumjua Mungu.

6 Lk 21:15;Yn 6:45;Yak 1:5Kwa kuwa BWANA huwapa watu hekima;

Kinywani mwake hutoka maarifa na ufahamu;

Veja também