3 Maana midomo ya malaya hudondosha asali,
Na kinywa chake ni laini kuliko mafuta;
4 Mhu 7:26;Ebr 4:12Lakini mwisho wake ni mchungu kuliko pakanga;
Ni mkali kama upanga wenye makali kuwili.
5 Ebr 13:4Miguu yake inateremkia mauti;
Hatua zake zinashikamana na kuzimu;
6 Hata asiweze kuiona njia sawa ya uzima;
Njia zake ni za kutangatanga wala hana habari.
7 Basi, wanangu, nisikilizeni sasa,
Wala msiache maneno ya kinywa changu.
8 Itenge njia yako mbali naye,
Wala usiukaribie mlango wa nyumba yake.
9 Usije ukawapa wengine heshima yako,
Na wakatili miaka yako;