8 Itenge njia yako mbali naye,
Wala usiukaribie mlango wa nyumba yake.
9 Usije ukawapa wengine heshima yako,
Na wakatili miaka yako;
10 Wageni wasije wakashiba nguvu zako;
Kazi zako zikawa ndani ya nyumba ya mgeni;
11 Nawe ukaziombolea siku zako za mwisho,
Nyama yako na mwili wako utakapoangamia;
12 Ukasema, Jinsi nilivyochukia maonyo,
Na moyo wangu ukadharau kukemewa;
13 Wala sikuisikia sauti ya waalimu wangu,
Wala sikuwategea sikio langu walionifundisha!
14 Nilikuwa karibu na kuingia katika maovu yote,
Katikati ya mkutano na kusanyiko.