6 Ayu 12:7Ewe mvivu, mwendee chungu,
Zitafakari njia zake ukapate hekima.
7 Kwa maana yeye hana kiongozi,
Wala msimamizi, wala mkuu,
8 Lakini hujiwekea akiba ya chakula wakati wa jua;
Hukusanya chakula chake wakati wa mavuno.
9 Ewe mvivu, utalala hadi lini?
Utaondoka lini katika usingizi wako?
10 Mit 24:33-34Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo,
Bado kukunja mikono upate usingizi!
11 Hivyo umaskini wako huja kama mnyang’anyi,
Na uhitaji wako kama mtu mwenye silaha.