Publicidade

Provérbios 6

6 Ayu 12:7Ewe mvivu, mwendee chungu,

Zitafakari njia zake ukapate hekima.

7 Kwa maana yeye hana kiongozi,

Wala msimamizi, wala mkuu,

8 Lakini hujiwekea akiba ya chakula wakati wa jua;

Hukusanya chakula chake wakati wa mavuno.

9 Ewe mvivu, utalala hadi lini?

Utaondoka lini katika usingizi wako?

10 Mit 24:33-34Bado kulala kidogo, kusinzia kidogo,

Bado kukunja mikono upate usingizi!

11 Hivyo umaskini wako huja kama mnyang’anyi,

Na uhitaji wako kama mtu mwenye silaha.

Veja também

Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-07-05_19-25-13-