Publicidade

Provérbios 14

1 Rut 4:11;Mit 24:3,4 Kila mwanamke aliye na hekima hujenga nyumba yake;

Bali aliye mpumbavu huibomoa kwa mikono yake mwenyewe.

2 Ayu 12:4 Yeye aendaye kwa unyofu wake humcha BWANA;

Bali aliye mkaidi katika njia zake humdharau.

3 Mit 12:6 Katika kinywa cha mpumbavu mna fimbo ya kiburi,

Bali midomo ya wenye hekima huwahifadhi.

4 Zizi ni safi ambapo hapana ng’ombe;

Bali nguvu za ng’ombe zaleta faida nyingi.

5 Kut 20:16 Shahidi mwaminifu hatasema uongo;

Bali shahidi wa uongo, pumzi zake ni uongo.

6 Mit 17:24 Mwenye dharau hutafuta hekima, asiipate;

Bali maarifa huwa mepesi kwa mwenye ufahamu.

7 Toka mbele ya uso wa mpumbavu,

Maana hutaona kwake midomo ya maarifa.

8 Lk 12:20;1 Kor 3:19 Akili za mwenye busara ni kujua njia yake;

Lakini upumbavu wa wapumbavu ni udanganyifu.

9 Mit 1:22 Wapumbavu huidharau hatia;

Bali upo upendeleo kwa wenye haki.

10 Moyo huujua uchungu wa nafsi yake,

Wala mgeni haishiriki furaha yake.

11 Ayu 8:15;Mit 3:33 Nyumba ya mtu mwovu itabomolewa;

Bali hema la mwenye haki litafanikiwa.

12 Mit 16:25;Rum 6:21 Iko njia ionekanayo kuwa sawa machoni pa mtu,

Lakini mwisho wake ni njia za mauti.

13 Mhu 2:2 Hata wakati wa kucheka moyo huwa na huzuni;

Na mwisho wa furaha ni uzito wa moyo.

14 Mit 12:14;2 Kor 1:12;Flp 4:7 Ageukaye moyoni hushiba njia zake mwenyewe;

Na mtu mwema ataridhika nafsini mwake.

15 Mjinga huamini kila neno;

Bali mwenye busara huangalia sana aendavyo.

16 Mit 22:3 Mwenye hekima huhadhari, na kujitenga na uovu;

Bali mpumbavu hupuuza yote, na hajali.

17 Yeye aonaye hasira upesi atatenda kwa ujinga;

Na mtu mwenye hila mbaya huzirwa.

18 Wajinga hurithi upumbavu;

Bali wenye busara huvikwa taji la maarifa.

19 Wabaya huinama mbele ya wema,

Na wasio haki malangoni mwao wenye haki.

20 Mit 19:7 Maskini huchukiwa hata na jirani yake;

Bali tajiri ana marafiki wengi.

21 Zab 41:1 Amdharauye mwenzake afanya dhambi;

Bali amhurumiaye maskini ana heri.

22 Je! Hawakosi wawazao mabaya?

Bali fadhili na kweli zina wao wawazao mema.

23 Katika kila kazi mna faida;

Bali maneno ya midomo huleta hasara tu.

24 Taji la wenye hekima ni mali zao;

Bali upumbavu wa wajinga ni upumbavu tu.

25 Shahidi wa kweli huponya nafsi za watu;

Bali atoaye uongo hudanganya.

26 Kumcha BWANA ni tumaini imara;

Watoto wake watakuwa na kimbilio.

27 Mit 13:14 Kumcha BWANA ni chemchemi ya uzima,

Ili kuepukana na tanzi za mauti.

28 Utukufu wa mfalme ni wingi wa watu wake;

Bali uchache wa watu ni uharibifu wa mkuu wao.

29 Mit 15:18;Mt 11:29;1 Kor 13:4,5;Yak 1:19 Asiye mwepesi wa hasira ana fahamu nyingi;

Bali mwenye roho ya hamaki hutukuza upumbavu.

30 Ayu 5:2;Zab 112:10;Mdo 7:9;Rum 1:29;Yak 4:5 Moyo ulio mzima ni uhai wa mwili;

Bali husuda ni ubovu wa mifupa.

31 Ayu 31:15,16;Mhu 5:8;Mit 17:5;22:2;Mt 25:40;1 Yoh 3:17 Amwoneaye maskini humsuta Muumba wake;

Bali yeye awahurumiaye wahitaji humheshimu.

32 Ayu 13:15;Zab 23:4;2 Kor 1:9;2 Tim 4:18 Mtu mbaya husukumwa chini katika kutenda mabaya kwake;

Bali mwenye haki ana matumaini katika kufa kwake.

33 Hekima hukaa katika moyo wake mwenye ufahamu;

Bali yaliyo ndani ya wapumbavu hudhihirika.

34 Haki huinua taifa;

Bali dhambi ni aibu ya watu wowote.

35 Mt 24:45-47 Upendeleo wa mfalme humwelekea mtumwa atendaye kwa busara;

Bali hasira yake itakuwa juu yake aletaye aibu.

Veja também

Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-07-05_19-25-13-