Publicidade

Provérbios 1

1 Mithali za Sulemani, mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli.

Utangulizi

2 Kujua hekima na adabu; kutambua maneno ya ufahamu; 3 kufundishwa matendo ya busara, katika haki na hukumu na adili. 4 Kuwapa wajinga werevu, na kijana maarifa na tahadhari; 5 mwenye hekima asikie na kuongezewa elimu, na mwenye ufahamu ayafikie mashauri yenye njia. 6 Kufahamu mithali na kitendawili, na maneno ya wenye hekima na mafumbo yao. 7 Kumcha BWANA ni chanzo cha maarifa, Bali wapumbavu hudharau hekima na adabu.

Veja também

Publicidade
Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-06-29_22-07-56-