1 Mithali za Sulemani, mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli.
Utangulizi
2 Kujua hekima na adabu; kutambua maneno ya ufahamu; 3 kufundishwa matendo ya busara, katika haki na hukumu na adili. 4 Kuwapa wajinga werevu, na kijana maarifa na tahadhari; 5 mwenye hekima asikie na kuongezewa elimu, na mwenye ufahamu ayafikie mashauri yenye njia. 6 Kufahamu mithali na kitendawili, na maneno ya wenye hekima na mafumbo yao. 7 Kumcha BWANA ni chanzo cha maarifa, Bali wapumbavu hudharau hekima na adabu.