Pular para o conteúdo
Publicidade

Provérbios 31

13 Hutafuta sufu na kitani;

Hufanya kazi yake kwa moyo wote.

14 Afanana na merikebu za biashara;

Huleta chakula chake kutoka mbali.

15 Rum 12:11;Mt 24:45;Lk 12:42Tena huamka, kabla usiku haujaisha;

Huwapa watu wa nyumbani mwake chakula;

Na wajakazi wake sehemu zao.

16 Huangalia shamba, akalinunua;

Kwa mapato ya mikono yake hupanda mizabibu.

17 Hujifunga nguvu viunoni kama mshipi;

Hutia mikono yake nguvu.

18 Huona kama bidhaa yake ina faida;

Taa yake haizimiki usiku.

19 Hutia mikono yake katika kusokota;

Na mikono yake huishika pia.

20 Huwakunjulia maskini mikono yake;

Naam, huwanyoshea wahitaji mikono yake.

Veja também