13 Hutafuta sufu na kitani;
Hufanya kazi yake kwa moyo wote.
14 Afanana na merikebu za biashara;
Huleta chakula chake kutoka mbali.
15 Rum 12:11;Mt 24:45;Lk 12:42Tena huamka, kabla usiku haujaisha;
Huwapa watu wa nyumbani mwake chakula;
Na wajakazi wake sehemu zao.
16 Huangalia shamba, akalinunua;
Kwa mapato ya mikono yake hupanda mizabibu.
17 Hujifunga nguvu viunoni kama mshipi;
Hutia mikono yake nguvu.
18 Huona kama bidhaa yake ina faida;
Taa yake haizimiki usiku.
19 Hutia mikono yake katika kusokota;
Na mikono yake huishika pia.
20 Huwakunjulia maskini mikono yake;
Naam, huwanyoshea wahitaji mikono yake.