Kusanyiko jipya la waliotawanyika
1 Mal 4:2Ondoka, uangaze; kwa kuwa nuru yako imekuja,
Na utukufu wa BWANA umekuzukia.
2 Maana, tazama, giza litaifunika dunia,
Na giza kuu litazifunika makabila ya watu;
Bali BWANA atakuzukia wewe,
Na utukufu wake utaonekana juu yako.
3 Ufu 21:24Na mataifa wataijia nuru yako,
Na wafalme kuujia mwanga wa mapambazuko yako.