Pular para o conteúdo
Publicidade

Isaya 52

Sayuni ishangilie

1 Nah 1:15;Isa 26:2;Ufu 21:2,27 Amka, amka, jivike nguvu zako, Ee Sayuni;

Jivike mavazi yako mazuri,

Ee Yerusalemu, mji mtakatifu;

Kwa maana tokea sasa hataingia ndani yako

Asiyetahiriwa, wala aliye najisi.

2 Zek 2:7 Jikung’ute mavumbi; uondoke,

Uketi, Ee Yerusalemu;

Jifungue vifungo vya shingo yako,

Ee binti Sayuni uliyefungwa.

3 Zab 44:12;1 Pet 1:18 Maana BWANA asema hivi, Mliuzwa bure; nanyi mtakombolewa bila fedha. 4 Maana Bwana MUNGU asema hivi, Watu wangu hapo kwanza walishuka Misri ili wakae huko kama wageni; na Mwashuri akawaonea bila sababu. 5 Rum 2:24 Basi sasa, nafanya nini hapa, asema BWANA, ikiwa watu wangu wamechukuliwa bure? Hao wanaowatawala wanapiga yowe, asema BWANA, na jina langu linatukanwa daima mchana kutwa. 6 Kwa hiyo watu wangu watalijua jina langu kwa hiyo watajua siku ile ya kuwa mimi ndimi ninenaye; tazama ni mimi.

7 Nah 1:15;Rum 10:15;Efe 6:15 Jinsi ilivyo mizuri juu ya milima

Miguu yake aletaye habari njema,

Yeye aitangazaye amani,

Aletaye habari njema ya mambo mema,

Yeye autangazaye wokovu,

Auambiaye Sayuni, Mungu wako anamiliki!

8 Sef 3:9 Sauti ya walinzi wako!

Wanapaza sauti zao, wanaimba pamoja;

Maana wataona jicho kwa jicho,

Jinsi BWANA arejeavyo Sayuni.

9 Pigeni kelele za furaha, imbeni pamoja,

Enyi mahali pa Yerusalemu palipokuwa ukiwa;

Kwa kuwa BWANA amewafariji watu wake,

Ameukomboa Yerusalemu.

10 Lk 3:6 BWANA ameweka wazi mkono wake mtakatifu

Machoni pa mataifa yote;

Na ncha zote za dunia

Zitauona wokovu wa Mungu wetu.

11 Yer 50:8;Ufu 18:4;2 Kor 6:17 Nendeni zenu, nendeni zenu, tokeni huko, msiguse kitu kichafu; tokeni kati yake; iweni safi ninyi mnaochukua vyombo vya BWANA. 12 Kut 12:33;14:19;Mik 2:13;Hes 10:25 Maana hamtatoka kwa haraka, wala hamtakwenda kwa kukimbia, kwa sababu BWANA atawatangulia; na Mungu wa Israeli atawafuata nyuma; awalinde.

Mtumishi atesekaye

13 Isa 42:1;Flp 2:9 Tazama, mtumishi wangu atatenda kwa busara, atatukuzwa, na kuinuliwa juu, naye atakuwa juu sana. 14 Zab 22:6;Isa 53:3 Kama vile wengi walivyokustaajabia, (uso wake ulikuwa umeharibiwa sana zaidi ya mtu yeyote, na umbo lake zaidi ya wanadamu), 15 Eze 36:25;Mdo 2:33;Ebr 9:13;Efe 3:5;Rum 15:21 ndivyo atakavyowastusha mataifa mengi; wafalme watamfumbia vinywa vyao; maana mambo wasiyoambiwa watayaona; na mambo wasiyoyasikia watayafahamu.

Estes versículos te tocaram? Ore agora!

+581 estão orando agora.

Junte-se à corrente de oração.

Veja também