6 Lk 2:11;Yn 3:16;Mt 28:18;1 Kor 15:25;Amu 13:18;Zab 45:3,6;Yer 23:6;Yn 1:1;Tit 2:13;Efe 2:14;Kol 1:20;Ebr 13:20Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa,
Tumepewa mtoto wa kiume;
Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake;
Naye ataitwa jina lake,
Mshauri wa Ajabu, Mungu Mwenye Nguvu,
Baba wa Milele, Mfalme wa Amani.
7 Dan 2:44;Lk 1:32-33Mamlaka ya enzi yake yatakuzwa daima,
Na kutakuwa na amani isiyo na mwisho,
Katika kiti cha enzi cha Daudi na ufalme wake;
Kuuthibitisha na kuutegemeza
Kwa hukumu na kwa haki,
Tangu sasa na hata milele.
Wivu wa BWANA wa majeshi ndio utakaotenda hayo.