Bildadi anena: Mtu awezaje kuwa mwenye haki mbele za Mungu
1 Ndipo Bildadi, Mshuhi, akajibu, na kusema,
2 Enzi na hofu zi pamoja na Mungu;25:2 Katika Kiebrania ni naye.
Hufanya amani katika mahali pake palipoinuka.
3 Mwa 1:3-5,14-16;Zab 19:4-6;139:8,11;Mt 5:45;Yak 1:17 Je! Majeshi yake yahesabika?
Ni nani asiyetokewa na mwanga wake?
4 Ayu 4:17;9:2;Zab 130:3;143:2;Rum 3:19,20 Basi mtu awezaje kuwa na haki mbele ya Mungu?
Au awezaje kuwa safi aliyezaliwa na mwanamke?
5 Tazama, hata mwezi hauangazi,
Wala nyota si safi machoni pake;
6 Zab 22:6 Seuze mtu, aliye mdudu!
Na mwanadamu, ambaye ni buu!