Publicidade

Jó 14

1 Ayu 15:14;Zab 51:5;Mhu 2:23 Mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke

Siku zake za kuishi si nyingi, naye hujaa taabu.

2 Isa 40:6;Yak 1:10;1 Pet 1:24 Yeye huchanua kama vile ua, kisha hukatwa;

Hukimbia kama kivuli, wala hakai kamwe.

3 Zab 144:3;143:2 Nawe, je! Wafumbua macho yako kumwangalia mtu kama yeye,

Na kunitia katika hukumu pamoja nawe?

4 Mwa 5:3;Zab 51:5;Yn 3:5;Rum 5:12;Efe 2:3 Ni nani awezaye kutoa kitu kilicho safi kitoke katika kitu kichafu? Hapana awezaye.

5 Kwa kuwa siku zake zimeamriwa, hesabu ya miezi yake unayo wewe,

Nawe umemwekea mipaka yake asiyoweza kuipita;

6 Zab 39:13 Acha kumwangalia yeye, apate kupumzika,

Hata atakapoitimiza siku yake, kama aliyeajiriwa.

7 Kwani yako matumaini ya mti, ya kuwa ukikatwa utachipuka tena,

Wala machipukizi yake hayatakoma.

8 Ijapokuwa mizizi yake huchakaa mchangani,

Na shina lake kufa katika udongo;

9 Lakini kwa harufu ya maji utachipuka,

Na kutoa matawi kama mche.

10 Lakini mwanadamu hufa, hufariki dunia;

Naam, mwanadamu hukata roho, naye yupo wapi?

11 Kama vile maji kupwa katika bahari,

Na mto kupunguka na kukatika;

12 Zab 102:26;Isa 51:6;Mdo 3:21;Rum 8:20;2 Pet 3:7;Ufu 20:14 Ndivyo mwanadamu hulala chini, asiinuke;

Hata wakati wa mbingu kutokuwako tena, hawataamka,

Wala kuamshwa usingizini.

13 Laiti ungenificha kuzimuni,

Ukanilinda kwa siri, hata ghadhabu zako zitakapopita,

Na kuniandikia muda ulioamriwa, na kunikumbuka!

14 Ayu 13:15;Zab 16:10;1 Kor 15:42-58;Flp 3:21 Mtu akifa, je! Atakuwa hai tena?

Mimi ningengoja siku zote za huduma yangu,

Hadi kufunguliwa kwangu kunifikie.

15 Ayu 13:22;Zab 50:4;Yn 5:28;1 The 4:16 Wewe ungeita, nami ningekujibu;

Ungekuwa na tamaa ya kazi ya mikono yako.

16 Kum 32:34;Ayu 10:6,14;13:27;Zab 56:8;Mit 5:21;Yer 32:19;Hos 13:12 Lakini sasa wazihesabu hatua zangu;

Je! Huchungulii dhambi yangu?

17 Kosa langu limetiwa mhuri mfukoni,

Nawe waufunga uovu wangu.

18 Lakini, tazama, mlima ukianguka hutoweka,

Nalo jabali huondolewa mahali pake;

19 Maji mengi huyapunguza mawe;

Mafuriko yake huuchukua mchanga wa nchi;

Nawe matumaini ya wanadamu wayaangamiza.

20 Wewe wamshinda nguvu sikuzote, naye hupita aende zake

Wabadili sura zake, na kumtuma aende mbali.

21 1 Sam 4:20;Zab 39:6;Mhu 9:5;Isa 63:16 Wanawe hufikia heshima, wala yeye hajui;

Kisha wao huaibishwa, lakini yeye hana habari zao.

22 Zab 49:14;Mit 14:32;Mt 8:12 Huhisi tu maumivu ya mwili wake,

Na huombolezea nafsi yake tu.

Veja também

Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-07-05_19-25-13-