Publicidade

Jó 4

Elifazi anena: Ayubu ametenda dhambi

1 Ndipo huyo Elifazi, Mtemani, akajibu na kusema,

2 Mtu akijaribu kuzungumza nawe, je! Utaona ni vibaya?

Lakini ni nani awezaye kujizuia asinene?

3 Tazama, wewe umewafunza watu wengi,

Nawe umeitia nguvu mikono iliyokuwa minyonge.

4 Maneno yako yamemtegemeza huyo aliyekuwa anaanguka,

Nawe umeyaimarisha magoti manyonge.

5 Mit 24:10;Lk 4:23 Lakini sasa haya yamekufikia wewe, nawe wafa moyo;

Yamekugusa, nawe wafadhaika.

6 Ayu 1:1;Mit 3:26 Je! Dini yako siyo tegemeo lako?

Na matumaini yako si huo uelekevu wa njia zako?

7 Kumbuka, tafadhali, ni nani aliyeangamia akiwa hana hatia?

Au ni wapi hao waelekevu walikatiliwa mbali?

8 Zab 7:14 Kama mimi nilivyoona, hao walimao maovu,

Na kupanda madhara, huvuna yayo hayo.

9 Kwa pumzi za Mungu huangamia.

Na kwa kuvuma kwa hasira zake humalizika.

10 Ayu 29:17;Zab 3:7 Kunguruma kwake simba, na sauti ya simba mkali,

Na meno ya simba wachanga, yamevunjika.

11 Zab 34:10 Simba mzee huangamia kwa kukosa mawindo,

Nao watoto wa simba jike wametawanyika mbalimbali.

12 Basi, nililetewa neno kwa siri,

Sikio langu likasikia manong’ono yake.

13 Ayu 33:15 Katika mawazo yaliyotoka katika maono ya usiku,

Hapo usingizi mzito uwaangukiapo wanadamu.

14 Hofu iliniangukia na kutetemeka,

Iliyoitetemesha mifupa yangu yote.

15 Zab 104:4;Mt 14:26;Ebr 1:14 Ndipo pepo ilipita mbele ya uso wangu;

Na nywele za mwili wangu zilisimama.

16 Hiyo pepo ilisimama kimya, nisiweze kutambua sura zake,

Mfano ulikuwa mbele ya macho yangu;

Kulikuwa kimya, nami nilisikia sauti, ikinena,

17 Je! Binadamu atakuwa na haki kuliko Mungu?

Je! Mtu atakuwa safi kuliko Muumba wake?

18 2 Pet 2:4 Tazama, yeye hawategemei watumishi wake;

Na malaika wake huwahesabia kosa;

19 Je! Si zaidi sana hao wakaao katika nyumba za udongo,

Ambazo misingi yao i katika mchanga,

Hao wanaopondwa kama nondo!

20 Kati ya asubuhi na jioni huvunjwa-vunjwa;

Waangamia milele wala hapana atiaye moyoni.

21 Je! Kamba ya hema yao haikung’olewa ndani yao?

Nao hufa hata bila kuwa na hekima.

Veja também

Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-07-05_19-25-13-