Ayubu ajibu: Hakuna mpatanishi
1 Ndipo Ayubu akajibu, na kusema,
2 Ayu 4:17;Zab 143:2;Rum 3:20Kweli najua kuwa ndivyo hivyo;
Lakini mtu huwaje mwenye haki mbele za Mungu?
3 Kama akipenda kushindana naye,
Hawezi kumjibu neno moja katika elfu.
4 Yeye ni mwenye hekima moyoni, na mwenye uwezo katika nguvu;
Ni nani aliyejifanya kuwa mgumu juu yake, naye akafanikiwa?