Publicidade

Jó 32

Elihu awakemea marafiki wa Ayubu

1 Basi hao watu watatu wakaacha kumjibu Ayubu, kwa sababu alikuwa mwenye haki machoni pake mwenyewe. 2 Mwa 22:21 Ndipo zikawaka hasira za huyo Elihu mwana wa Barakeli, Mbuzi, katika jamaa ya Ramu, juu ya Ayubu, kwa sababu alikuwa amejipa haki mwenyewe zaidi ya Mungu. 3 Tena hasira zake ziliwaka juu ya hao rafiki zake watatu kwa sababu hawakupata jawabu, lakini wamemhukumia Ayubu makosa. 4 Basi huyo Elihu alikuwa anangoja ili anene na Ayubu, kwa sababu hao wengine walikuwa wazee kuliko yeye. 5 Hata Elihu alipoona kuwa hapana jawabu katika vinywa vya watu hao watatu, hasira zake ziliwaka.

6 Basi Elihu mwana wa Barakeli, Mbuzi, akajibu, na kusema,

Mimi ni kijana, na ninyi ni wazee sana;

Kwa hiyo nilijizuia, nisithubutu kuwaonesha nionavyo.

7 Ayu 8:8,9 Nilisema, Yafaa siku ziseme,

Na wingi wa miaka ufundishe hekima.

8 1 Fal 3:9 Lakini hakika imo roho ndani ya mwanadamu,

Na pumzi ya Mwenyezi ndiyo impayo ufahamu.

9 1 Kor 1:21 Sio wakuu walio wenye hekima,

Wala sio wazee watambuao haki.

10 Basi nilisema, Nisikilizeni mimi;

Mimi nami nitawaonesha nionavyo.

11 Tazama, niliyangojea maneno yenu,

Nilizisikiliza nisikie hoja zenu,

Hapo mlipokitafuta mtakalonena.

12 Mit 18:13 Naam, niliwasikiza ninyi,

Na tazama, hapana mmoja aliyemshinda Ayubu,

Wala kumjibu maneno yake, kati yenu.

13 Yer 9:23 Jitunzeni msiseme, Sisi tumepata hekima;

Mungu huenda akamshinda, si mtu;

14 Kwa kuwa yeye hajayaelekeza maneno yake kwangu;

Wala sitamjibu mimi kwa maneno yenu.

15 Wameshangaa, hawajibu tena;

Hawana neno la kusema.

16 Na mimi, je! Ningoje, kwa sababu hawaneni,

Kwa sababu wasimama kimya, wala wasijibu tena;

17 Mimi nami nitajibu sehemu yangu,

Mimi nami nitaonesha nionavyo.

18 Kwa kuwa nimejaa maneno;

Roho iliyo ndani yangu hunihimiza.

19 Tazama, tumbo langu ni kama divai iliyozibwa;

Kama viriba vipya liko karibu kupasuka.

20 Nitanena, ili nipate kutulia;

Nitafunua midomo yangu na kujibu.

21 Tafadhali, nisiupendelee uso wa mtu;

Wala sitajipendekeza kwa mtu yeyote.

22 Mdo 12:22,23 Kwa kuwa mimi sijui kujipendekeza;

Au Muumba wangu angeniondoa kwa upesi.

Veja também

Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-07-05_19-25-13-