6 Bwana huwalinda wanyenyekevu,
nilipokuwa katika shida kubwa, aliniokoa.
7 Ee nafsi yangu, tulia tena,
kwa kuwa Bwana amekuwa mwema kwako.
8 Kwa kuwa wewe, Ee Bwana,
umeniokoa nafsi yangu na mauti,
macho yangu kutokana na machozi,
miguu yangu kutokana na kujikwaa,
9 ili niweze kutembea mbele za Bwana,
katika nchi ya walio hai.