Kutii Sheria Ya Bwana
9 Kijana aifanye njia yake kuwa safi jinsi gani?
Ni kwa kutii, akilifuata neno lako.
10 Ninakutafuta kwa moyo wangu wote,
usiniache niende mbali na amri zako.
11 Nimelificha neno lako moyoni mwangu
ili nisikutende dhambi.
12 Sifa ni zako, Ee Bwana,
nifundishe maagizo yako.
13 Kwa midomo yangu nitasimulia sheria zote
zinazotoka katika kinywa chako.
14 Ninafurahia kufuata sheria zako
kama mtu afurahiaye mali nyingi.
15 Ninatafakari maagizo yako
na kuziangalia njia zako.
16 Ninafurahia maagizo yako,
wala sitalipuuza neno lako.Bwana