Pular para o conteúdo
Publicidade

Zaburi 121

Bwana Mlinzi Wetu

Wimbo wa kwenda juu.

1 Nayainua macho yangu nitazame vilima,

msaada wangu utatoka wapi?

2 Msaada wangu hutoka kwa Bwana,

Muumba wa mbingu na dunia.

3 Hatauacha mguu wako uteleze,

yeye akulindaye hatasinzia,

4 hakika, yeye alindaye Israeli

hatasinzia wala hatalala usingizi.

5 Bwana anakulinda,

Bwana ni uvuli wako mkono wako wa kuume,

6 jua halitakudhuru mchana,

wala mwezi wakati wa usiku.

7 Bwana atakukinga na madhara yote,

atayalinda maisha yako,

8 Bwana atakulinda unapoingia na unapotoka,

tangu sasa na hata milele.

Veja também