Thawabu Ya Kumtii Bwana
Wimbo wa kwenda juu.
1 Heri ni wale wote wamchao Bwana,
waendao katika njia zake.
2 Utakula matunda ya kazi yako;
baraka na mafanikio vitakuwa vyako.
3 Mke wako atakuwa kama mzabibu uzaao
ndani ya nyumba yako;
wana wako watakuwa kama machipukizi ya mizeituni
kuizunguka meza yako.