1 Ee Bwana, umenichunguza
na kunijua.
2 Unajua ninapoketi na ninapoinuka;
unatambua mawazo yangu tokea mbali.
3 Unafahamu kutoka kwangu na kulala kwangu;
unaelewa njia zangu zote.
4 Kabla neno halijafika katika ulimi wangu,
wewe walijua kikamilifu, Ee Bwana.