7 Niende wapi nijiepushe na Roho yako?
Niende wapi niukimbie uso wako?
8 Kama nikienda juu mbinguni, wewe uko huko;
nikifanya vilindi139:8 Vilindi ina maana ya Kuzimu, ambayo ni Sheol kwa Kiebrania. kuwa kitanda changu,
wewe uko huko.
9 Kama nikipanda juu ya mbawa za mapambazuko,
kama nikikaa pande za mbali za bahari,
10 hata huko mkono wako utaniongoza,
mkono wako wa kuume utanishika kwa uthabiti.