1 Msifuni Bwana.
Mwimbieni Bwana wimbo mpya,
sifa zake katika kusanyiko la watakatifu.
3 Na walisifu jina lake kwa kucheza
na wampigie muziki kwa matari na kinubi.
4 Kwa maana Bwana anapendezwa na watu wake,
anawavika wanyenyekevu taji ya wokovu.
5 Watakatifu washangilie katika heshima hii,
na waimbe kwa shangwe vitandani mwao.