1 Bwana na akujibu unapokuwa katika dhiki,
jina la Mungu wa Yakobo na liwe kinga yako.
2 Na akutumie msaada kutoka patakatifu
na akupatie msaada kutoka Sayuni.
3 Na azikumbuke dhabihu zako zote,
na azikubali sadaka zako za kuteketezwa.
4 Na akujalie haja ya moyo wako,
na aifanikishe mipango yako yote.