Furaha Ya Msamaha
1 Heri mtu yule ambaye amesamehewa makosa yake,
ambaye dhambi zake zimefunikwa.
2 Heri mtu yule ambaye Bwana
hamhesabii dhambi,
na ambaye rohoni mwake
hamna udanganyifu.
3 Niliponyamaza, mifupa yangu ilichakaa
kwa kulia kwa maumivu makali mchana kutwa.
4 Usiku na mchana
mkono wako ulinilemea,
nguvu zangu zilinyonywa
kama vile katika joto la kiangazi.
5 Kisha nilikujulisha dhambi yangu
wala sikuficha uovu wangu.
Nilisema, "Nitaungama
makosa yangu kwa Bwana."
Ndipo uliponisamehe
hatia ya dhambi yangu.
6 Kwa hiyo kila mtu mcha Mungu akuombe
wakati unapopatikana,
hakika maji makuu yatakapofurika
hayatamfikia yeye.