7 Upendo wako usiokoma
ni wa thamani mno!
Watu wakuu na wadogo
hujificha uvulini wa mbawa zako.
8 Wanajifurahisha katika wingi nyumbani mwako,
nawe utawanywesha katika mto wa furaha zako.
9 Kuwa pamoja nawe ni kijito cha uzima,
katika nuru yako twaona nuru.