Maombi Ya Mtu Mgonjwa
Kwa mwimbishaji. Zaburi ya Daudi.
1 Heri mtu yule anayemjali mnyonge,
Bwana atamwokoa wakati wa shida.
2 Bwana atamlinda na kuyahifadhi maisha yake,
atambariki katika nchi
na hatamwacha katika tamaa ya adui zake.
3 Bwana atamtegemeza awapo mgonjwa kitandani,
atamwinua kutoka kitandani mwake.