Pular para o conteúdo
Publicidade

Salmos 51

7 Nioshe kwa hisopo, nami nitakuwa safi,

unisafishe, nami nitakuwa mweupe kuliko theluji.

8 Unipe kusikia furaha na shangwe,

mifupa uliyoiponda na ifurahi.

9 Ufiche uso wako usizitazame dhambi zangu,

na uufute uovu wangu wote.

10 Ee Mungu, uniumbie moyo safi,

uifanye upya roho ya uthabiti ndani yangu.

11 Usinitupe kutoka mbele zako

wala kuniondolea Roho wako Mtakatifu.

12 Unirudishie tena furaha ya wokovu wako,

unipe roho ya utii, ili initegemeze.

Veja também