Upendo wa Mwenyezi Mungu
Zaburi ya Daudi.
1 Ee nafsi yangu, umhimidi Mwenyezi Mungu.
Vyote vilivyo ndani yangu
vilihimidi jina lake takatifu.
2 Ee nafsi yangu, umhimidi Mwenyezi Mungu,
wala usisahau wema wake wote:
3 akusamehe dhambi zako zote,
akuponya magonjwa yako yote,
4 aukomboa uhai wako na kaburi,
akuvika taji la upendo na huruma,