Pular para o conteúdo
Publicidade

Salmos 119

Kutii Torati ya Mwenyezi Mungu

9 Kijana aisafishe njia yake jinsi gani?

Ni kwa kutii, akilifuata neno lako.

10 Ninakutafuta kwa moyo wangu wote,

usiniache niende mbali na amri zako.

11 Nimelificha neno lako moyoni mwangu

ili nisikutende dhambi.

12 Uhimidiwe, Ee Mwenyezi Mungu;

nifundishe maagizo yako.

13 Kwa midomo yangu nitasimulia sheria zote

zinazotoka katika kinywa chako.

14 Ninafurahia kufuata sheria zako

kama mtu afurahiaye mali nyingi.

15 Ninatafakari maagizo yako

na kuziangalia njia zako.

16 Ninafurahia maagizo yako,

wala sitalipuuza neno lako.

Veja também