Publicidade

Salmos 128

Thawabu ya kumtii Mwenyezi Mungu

1 Heri wale wote wamchao Mwenyezi Mungu,

wanaoenda katika njia zake.

2 Utakula matunda ya kazi yako;

baraka na mafanikio vitakuwa vyako.

3 Mke wako atakuwa kama mzabibu uzaao

ndani ya nyumba yako;

wana wako watakuwa kama machipukizi ya mizeituni

kuizunguka meza yako.

4 Hivyo ndivyo atakavyobarikiwa

mtu amchaye Mwenyezi Mungu.

Veja também

Bíblia Online Bíblia Online

Bíblia Online • Versão: 2026-07-05_19-25-13-