11 Watasimulia utukufu wa ufalme wako
na kusema kuhusu ukuu wako,
12 ili watu wote wajue matendo yako makuu
na utukufu wa fahari ya ufalme wako.
13 Ufalme wako ni ufalme wa milele,
mamlaka yako hudumu vizazi vyote.
Mwenyezi Mungu ni mwaminifu kwa ahadi zake zote
na mwenye upendo kwa vyote alivyovifanya.